MRISHO MPOTO: Nilijua leo tungeambiwa Roma amepatikana
Mrisho
Mpoto anasema alikwenda leo asubuhi na mapema akiwa na matarajio kuwa
huenda polisi leo wangeweza kuwapa taarifa kuwa wasanii hao wamepatikana
lakini kwa mujibu wa taarifa ya Kamishna Simon Sirro ni kwamba mpaka
sasa wasanii hao hawajapatikana na hawafahamiki wapo wapi, ila amesema
bado wanaendelea na upelelezi.
Mbali na hilo Mrisho Mpoto ametoa wito kwa jamii
"Sisi kama wasanii
tunaendelea kusikitishwa na kuumizwa na suala zima la Roma Mkatoliki na
ndiyo maana nimekuja hapa asubuhi na mapema nilikuwa najua kwamba
tutaambiwa Roma amepatikana yupo hapa salama na vitu kama hivyo, kwa
hiyo matarajio na nilichokisikia vimetofautiana lakini siwezi kuingilia
mamlaka," alisema Mrisho Mpoto
Mbali na hilo Mrisho Mpoto ametoa wito kwa jamii
"Wito wangu kwa jamii ni
utulivu na kuendelea kumuomba Mungu na kuacha waandishi wa habari na
vyombo husika viweze kufanya kazi zake" alisema Mrisho Mpoto
0 comments: