Marekani
imefanya mashambulizi ya anga katika kambi ya jeshi la Syria katika
kujibu mapigo ya tukio linalodaiwa kuwa shambulizi la silaha za kemikali
dhidi ya raia katika mji unaoshikiliwa na waasi.Makombora 59 aina ya
Tomahawk yamerushwa kutoka kwenye meli mbili za kijeshi kutoka bahari ya
Mediterranean.Rais Donald Trump amesema wameshambulia kambi ya jeshi ya
Shayrat ambayo ilifanya mashambulizi ya kemikali siku ya jumanne.
Hili ni
shambulizi la kwanza la Marekani moja kwa moja dhidi ya serikali ya
Syria. Urusi ambayo inamuunga mkono rais Bashar al-Assad, imeshutumu
shambulizi hilo.
Kambi ya jeshi ya Shayrat inavyoonekana baada ya mashambulizi
Meli ya jeshi la Marekani ikirusha makombora ya Tomahawk
Learn more »